

Tofauti Ya Kazi Na Wito
Umewahi kujiuliza kuna tofauti gani kati ya wito na kazi? Ingawa watu wengi wanachanganya maana ya maneno haya mawili muhimu katika maisha na kujikuta wanazungumzia wito mahali pa kazi na kuzungumzia kazi mahali pa wito,ipo tofauti kubwa kati ya kazi na wito.

Badili Uchungu Kuwa Wito
Umewahi kumsamehe mtu aliyekukosea bila kuangalia ukubwa wa kosa alilokufanyia hata kama anaendelea kukukosea?. Mwezi wa pili mwaka 1993 Marry Johnson alipokuwa kazini alipokea simu yenye taarifa mbaya ikimjulisha kuhusu kifo cha mwanaye wa pekee Laramiun Bry ambaye alikuwa ameuawa kikatiri na muuaji Oshea Israel huko nchini Marekani.

Ujinga Siyo Kitu Kibaya tu!
Ingawa ujinga siyo lazima kuwa kitu kibaya,katika hali ya kawaida hakuna mtu ambaye angependa kuitwa mjinga.Umewahi kuona watu wakigombana na amani kuvurugika kwa kuwa tu mmoja amemwita mwenzake mjinga?

William Kamkwamba-Kutoka Umasikini Hadi Utajiri.
Hakutazama hali ya umaskini uliokuwa unamzunguka yeye na familia yake zaidi ya kuangalia ni namna gani angeweza kutumia kitu pekee ambacho Mungu amempa ambacho ni kipaji na ubunifu kujikwamua yeye,familia na jamii inayomzunguka.

Mambo 4 Ya Kufanya Ukipatwa Na Janga.
Umewahi kupatwa au kukutana na jambo au janga lolote maishani? Au kama siyo wewe labda umewahi kumwona mtu ambaye amefikwa na janga kubwa? Ingawa majanga yanatofautiana kwa ukubwa binadamu wengi wamewahi kukutana au kufikwa na janga kubwa au dogo.

Hakuna Jambo Lisilowezekana
Unakumbuka moja ya makala zangu ambayo nimewahi kuandika kwenye mtandao huu inayoitwa “kuna fursa katika kila hali? Ukiunganisha na dhana ya maisha ni fursa ambayo haina mipaka na hiki ninachokwenda kukushirikisha leo utakubaliana nami kabisa kuwa kila hali imeficha fursa.

Alianza Kinyonge Akamaliza kwa Ushindi!
Je umeshindwa mara ngapi katika maisha yako? Jamaa alishindwa kuuza bidhaa yake ya kuku wa kukaanga mara 1009, alikuwa ni mtu ambaye hajawahi kufurahia maisha hata kidogo. Alipojaribu kuuza mapishi yake ya kuku kwa mikahawa na wafanyabiashara, wengi walimkataa, lakini hakukata tamaa. Hatimaye, alifanikiwa kuanzisha biashara yake ambayo sasa ni moja ya mifumo mikubwa ya chakula cha haraka duniani.

Pesa Siyo Msingi Pekee wa Mafanikio
Kuna kitu kimoja kinachonishangaza kila mara—watu wanapata pesa, lakini wanazichezea. Ni kama hawaoni fursa zilizo mbele yao. Badala ya kuzitumia kubadilisha maisha yao na ya familia zao, wanazitelekeza kama maji yaliyomwagika chini.

Anza Na Tabia Kubadilika
“Natamani kubadilika na kuboresha maisha yangu katika eneo fulani,lakini nafika mahali nashindwa naendelea kufanya kitu ambacho sikipendi inaniumiza sana” Hebu fikiri unakutana na mtu anakushirikisha shida yake kwa maneno uliyotangulia kusoma hapo juu utamsaidiaje?

Muda Na Mabadiliko
Tangu tusherehekee January 1 kuupokea mwaka 2024 wala si muda mrefu sana.Ilianza siku,ikatengeneza wiki,nayo wiki ikatengeneza mwezi na mwisho miezi ikatengeneza jumla ya miezi 12 ambayo kwa pamoja imepewa jina la mwaka 2024.
Kinachoniumiza mwenzenu siyo mwaka kwisha kwa sababu 2024 siyo mwaka wa kwanza kwisha,kuna miaka mingi imekuja na kupita;ila kila ninapotafakari kuwa sitakaa nikuone tena mwaka 2024 pamoja na miezi yako mpaka nitakapomaliza safari yangu katika dunia hii inanitisha.

Maneno Huumba!
“Mungu hukupa kile unachoomba” Umewahi kusikia huu msemo ukitumiwa na watu wengi? Ni vigumu kujua kama watu wengi wanaotumia hii misemo wanaujua ukweli na maana yake au wanaitumia tu kwa sababu imezoeleka katika jamii!

Kesho Ya Manyani - Hadithi Ya Maamuzi
Mvua ilinyesha kwa nguvu, kama vile mawingu yalikuwa yamemimina mapipa ya maji moja kwa moja kutoka angani. Manyani walihangaika—kila mmoja akitafuta mahali pa kujificha na kuwalinda watoto wake dhidi ya mvua kali. Lakini juhudi zao zilionekana kugonga mwamba. Hakukuwa na mahali pa uhakika, kila mmoja akihangaika kwa njia yake.

Nguvu Ya Imani Katika Kila Unalofanya
Je, unawahi kufikiri kuhusu jinsi dunia tunayoishi inaongozwa na kanuni na sheria zisizobadilika? Kama zilivyo sheria za kisheria zilizoundwa na binadamu ili kuweka utaratibu wa maisha, vivyo hivyo kuna sheria za asili zinazoongoza mafanikio na maendeleo yetu. Sheria hizi haziwezi kuvunjwa bila madhara—ukizivunja, basi matokeo yake yatakuathiri kwa njia moja au nyingine.

MIMI Naitwa Muda Mnitumie Vizuri!
Mimi naitwa MUDA,ndio naitwa Muda ndilo jina langu.Nimesubiri kutambulishwa leo nimechoka kusubiri nimeamua kuvunja huo mwiko najitambulisha mwenyewe mimi naitwa Muda. Kutokunifahamu vizuri kumesababisha mkanganyiko na majuto makubwa kwa wanadamu wengi.

Ulishinda Kabla Ya Kuzaliwa
Kila mtu anatamani kutambulika na jamii kuwa ni mshindi katika jambo lolote ambalo angeweka mkono maishani mwake.Lakini matokeo huwa kinyume, wanaoshinda ni wachache na idadi ya wanaosajiliwa upya katika daftari la wanaoshindwa inaongezeka kila siku.

Tatizo Siyo Fursa
Unawaza nini ndani mwako unapofika mahali umekwama katika mazingira fulani kimaisha? Iwe umefukuzwa kazi uliyokuwa unaitegemea kuendesha maisha,umemaliza shule na unahangaika kutafuta kazi bila mafanikio? Unaona huo kuwa kama mwisho wa kila kitu na milango yote kufungwa au unaona kama ndiyo mwanzo wa milango mingine iliyokuwa haijakufungukia kufungukia sasa?

Jinsi Ya Kujiongeza Thamani
Watu wengi usiku na mchana wanahangaika kutafuta pesa kama njia ya kuwawezesha kumiliki zaidi wakiamini kwa kufanya hivyo wako katika njia sahihi ya kuyaelekea mafanikio. Huduma na kazi nyingi za wito zimeishia njiani baada ya watu kukosea mahali pa kuanzia kwa kutoa kwanza kipaumbele kwenye mafanikio ya pesa na kufanya wito kuwa kipaumbele cha pili matokeo yake wanapishana na pesa.

Wewe Ni Nani?
Wewe ni nani kwa hakika? Je, kuna jina unalolipenda kuitwa? Je, mara nyingi watu wanakutambua kwa sifa gani? Wewe mwenyewe unajiita nani? Hii ndiyo sehemu ya utambulisho wetu ambayo mara nyingi huwa hatuisemi hadharani. Lakini hebu tuangalie jinsi utambulisho huu unavyoweza kuleta tofauti kubwa katika maisha yetu.

Unao Uwezo Kushinda Vikwazo.
Je, umewahi kujiuliza namna gani watu wengine wanavyotumia uwezo wao kufikia mafanikio makubwa, huku wengine wakiendelea kusuasua na kubaki na ndoto zao? Je, unadhani uwezo wa kipekee ulionao unaweza kuchochewa na kufikia vipindi vipya vya mafanikio? Ni ukweli usiopingika kwamba kila mmoja wetu ana uwezo wa ndani, lakini je, unajua siri ya jinsi watu wenye mafanikio wanavyotumia uwezo wao?

Tafuta Elimu Kwanza: Kabla Ya Kutamani Kumiliki Pesa Zaidi.
Umewahi kukaa chini ukajiuliza kwa nini mtu mmoja ana uwezo wa kumiliki pesa nyingi wala hata kuhangaika na mwingine pesa kidogo tu ikiingia mkononi mwake hatulii mpaka hiyo hela itakapokwisha au ikibaki kiasi fulani basi anatulia?